• HATUA ILI UWEZE KUPATA HATIMILIKI YA KIWANJA AU SHAMBA LAKO

    Related image
    Karibuni ndugu wasomaji wangu wa blog yetu pendwa ya Manyanya Engineering.Leo napenda kutoa elimu juu ya hatua kadhaa za kufata ili uweze kupima kiwanja chako au shamba lako na uweze kupatiwa hatimiliki.


    Somo hili ni muhimu sana ukizingatia kipindi hiki ambacho rasilimali ardhi imekuwa adimu sana na ghari mno hivyo unyang’anyi na wizi katika ardhi umekuwa ni wa hali ya juu.
    HATIMILIKI ni hati inayompa mtu haki ya kisheria ya kumiliki ardhi kwa kipindi maalumu.
    PITA NAMI SASA KATIKA MADA YETU YA LEO:
    1 Ukaguzi wa eneo lako husika.
    Ili kujua eneo lako limepangwa kwa ajili ya matumizi gani, Hapa atashirikishwa mpima ardhi kwa ajili ya kufanya utambuzi wa eneo husika kujua lipo kwa ajili ya matumizi gani, Hivyo ni lazima afike site kwako na kifaa (Handheld GPS), Achukue vipimo kuzunguka eneo lako, Baada ya hapo akatafute taarifa za eneo lako halmashaur/ wizaran ili aweze kupata raman ya mipango miji.

    Global Position System (Handled GPS)

    2 Matokeo ya zoezi la ukaguzi wa eneo,
     Eneo husika kukosa sifa za kupimika,
    eneo husika linaweza kukosa sifa za kupimika endapo eneo hilo kuwa limeandaliwa matumizi ya kijamii (halina mchoro wa mipango miji) mfano makabuli, barabara, soko n.k
     Eneo husika kuwa na sifa ya kupimika,
    Eneo husika kuwa katika matumizi ambayo mtu binafsi anaweza kumili mfano makazi, hotel, biashara n.k

    Viwanja kwa matumizi ya kijamii
    3 Kibali cha upimaji,
    Mteja au mmiliki halali wa eneo husika inabidi aandae barua kwa ajili ya kuomba kupimiwa eneo lake, Barua hiyo itapita serikali ya mtaa na halmashauri husika.

    mfano wa barua

    4.Upimaji,
    Hapa ni suala la kitaaluma zaidi ambapo mtaalam ataweka mipaka katika eneo lako kwa kutumia mawe (beacons), litaandaliwa file kwa ajili ya kwenda wizaran likiambatanishwa na ramani ya upimaji. Na mwishowe utarudishiwa ramani iliyo hakikiwa toka wizarani kama ramani ya upimaji.
    zoezi la upimaji ardhi litafanyika

    5 Mteja utakabiziwa ramani ya upimaji,
    ambayo utapaswa uende nayo kwenye halmashaur husika umuone afisa ardhi ili aweze kukuandalia hati miliki yako.
                    mfano wa hati 

    Mpaka hapo ndugu msomaji utakuwa una miliki eneo lako husika na hapo hakuna yeyote atakaeweza kukusumbua .
    v  Ni matumaini yangu utakuwa umepata picha juu ya HATIMILIKI na endapo kuna swali usisite kuwasiliana nasi.Karibu sana!!



  • 0 comments:

    Post a Comment

    HAVE YOU RECOMMENDED TO USE GREAT PERSON?

    Yes, now here you are at the right place.Meet with innovative,creative and multi-purpose engineer.

    ADDRESS

    P.o.Box 5848,Tanga,
    TANZANIA

    EMAIL

    omarisaidi77@gmail.com

    TELEPHONE

    +25527 2646279

    MOBILE

    +255753629218
    +255689636501
    +255657781613